Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Thursday 18 April 2013

Mugabe:Wamagharibia wasiingilie uchaguzi ujao

Rais Gabriel Robert Mugabe wa Zimbabwe amesema hatoruhusu wageni kuingilia zoezi la uchaguzi mkuu ujao na badala yake amewataka Wamagharibi kuheshimu uhuru wa kujitawala wa nchi yake. Akizungumza leo Alhamisi wakati wa kuadhimisha miaka 33 ya uhuru wa Zimbabwe, Rais Mugabe amesema nchi ambazo zimefungua milango kwa Wamagharibi kujipenyeza zimeendelea kubaki nyuma kimaendeleo. Kiongozi huyo ametoa wito kwa Wazimbabwe kujitokeza kwa wingi wakati wa uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika kati ya mwezi Juni na Septemba mwaka huu. Pia amesema wananchi wako huru kumchagua kiongozi yeyote wampendaye. Amewahakikishia Wazimbabwe kwamba uchaguzi huo utakuwa huru na wa haki. Inafaa kukumbusha hapa kuwa uchaguzi mkuu ujao nchini Zimbabwe utakuwa wa kwanza chini ya katiba mpya na utaashiria mwisho wa serikali ya umoja wa kitaifa iliobuniwa mwaka 2009 ambapo Rais Mugabe alilazimika kugawana madaraka na hasimu wake wa muda mrefu, Morgan Tsvangirai.

0 comments:

Post a Comment