Mkuu wa jopo la Maualaa nchini Somalia, ameponea chupuchupu kuuawa
katika mripuko uliotokea leo mjini Mogadishu. Sheikh Bashir Ahmed Salad
ameokoka na kifo licha ya kutokea mripuko ndani ya gari yake katika eneo
la Hodan, kusini mwa mji mkuu wa Somalia, Mogadishu, bali hata
hakujeruhiwa katika mripuko huo. Hadi sasa hakuna kundi lolote
lililotangaza kuhusika na shambulio hilo ingawa kundi la ash Shabab
linadhaniwa kuhusika na shambulio hilo. Kundi la ash Shabab ambalo bado
linadhibiti baadhi ya maeneo ya katikati na kusini mwa Somalia, kwa mara
kadhaa limekuwa likifanya mashambulizi dhidi ya vikosi vya serikali na
vile vya Umoja wa Afrika AMISOM katika mji mkuu wa nchi hiyo Mogadishu.
Sikiliza Live
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment