Shirika la ndege la Lufthansa linalomilikiwa na serikali ya
Ujerumani limelazimika kufutilia mbali safari za ndani ya nchi, zile za
bara Ulaya na hata za kimataifa kutokana na mgomo wa wafanyakazi wake
wakiwemo marubani.
Lufthansa ambalo ni miongoni mwa mashirika makubwa ya
usafiri wa ndege duniani linakabiliwa na matatizo makubwa ya fedha na
wafanyakazi wameamua kugoma ili kuishinikiza serikali kuboresha
mazingira yao ya kazi pamoja na kuongezwa mishahara yao.
Wataalamu wa masuala ya uchumi wanasema mgomo huo ulioanza
leo utaisababishia Ujerumani hasara ya mamilioni ya dola na hivyo
kuyumbisha zaidi uchumi wa Ulaya.
Mazungumzo kati ya wafanyakazi wa shirika hilo na serikali
kuhusu nyongeza ya mishahara yamefanyika katika duru tatu na kumalizika
bila ya makubaliano yoyote
0 comments:
Post a Comment