Msemaji wa kundi la waasi wa M23 ametangaza kuwa mazungumzo
ya amani kati ya kundi hilo na serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya
Kongo yameanza katika mji mkuu wa Uganda, Kampala.
Duru za habari kutoka Kampala zimearifu kuwa, Rene Abandi
anaongoza ujumbe wa waasi wa M23 kwenye mazungumzo hayo na kwamba pande
mbili zimekutana na mpatanishi wa Uganda katika vikao tofauti.
Mazungumzo hayo yalianza Disemba mwaka uliopita chini ya
usimamizi wa taasisi ya eneo la Ukanda wa Maziwa Makuu ya Afrika lakini
yalisimama mwishoni mwa mwezi Februari kutokana na sababu mbalimbali.
Harakati ya M23 inahesabiwa kuwa kundi kubwa zaidi la waasi
huko Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na mwaka uliopita
lilizusha mgogoro mkubwa na mapigano kwenye eneo hilo.
0 comments:
Post a Comment