Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba,
amewataka wakazi wa Mkoa wa Tanga, kushikamana ili kufufua uchumi wao,
nyinginevyo mkoa huo unaweza kuwa wa mwisho katika ukusanyaji wa pato la
taifa.
Pamoja na kuwa na bandari na reli, mkoa huo una fursa nyingi za kuwezesha kuchangis kwa kiwango kikubwa katika pato la taifa.
Akizungumza katika kongamano la kufufua uchumi wa
Mkoa wa Tanga juzi, Profesa Lipumba alisema wenyeji wa mkoa huo ndio
wenye dhamana na jukumu la kusimamia maendeleo yao.
Alisema bandari na viwanda kadhaa vilivyoko mkoani
humo, ni sehemu ya rasilimali za kuiwezesha Tanga kupiga hatua za
kimaendeleo na hasa katika uchumi.
“Lakini pia kuongeza ajira kwa vijana wa ndani na
nje ya mkoa huo, kwa hiyo watu wa Tanga lazima mshikamane kama mnataka
kupiga hatua za kiuchumi,” alisisitiza.
Lipumba alisema Mkoa wa Tanga kwa nyuma
kimaendeleo kunatokana na viongozi wake walioko Serikalini, kuendeleza
ubinafsi na kuacha kuzitumia nafasi zao kupigania maendeleo.
Akizungumza katika kongamano hilo, Mbunge wa Bunge
la Afrika ya Mashariki, Twaha Issa Taslima, alisema Mkoa wa Tanga
unaweza kupiga hatua kibiashara ikiwa tu utazitumia fursa zilizopo hasa
baada ya kufunguliwa kwa Soko la Pamoja la Afrika ya Mashariki.
Aliwataka wafanyabiashara kulitumia soko hilo kwa
uwezo wao wote kwa kuzingatia kuwa litawawezesha kupiga hatua kubwa za
kimaendeleo.
0 comments:
Post a Comment