Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Saturday 13 April 2013

Jaji ajiondoa kusikiliza kesi ya dikteta wa Misri

 Jaji Mostafa Hassan Abdullah wa mahakama ya jinai ya mjini Cairo, Misri amejiondoa kusikiliza kesi ya mauaji iliyofunguliwa tena dhidi ya dikteta wa zamani wa nchi hiyo Hosni Mubarak na kuamua kuihamishia kesi hiyo kwenye mahakama ya rufaa. Jaji huyo aliyekuwa amepangiwa kusikiliza tena kesi inayomkabili Hosni Mubarak, waziri wake wa zamani wa Mambo ya Ndani Habib al-Adly pamoja na maafisa wengine wanne waandamizi wa utawala wake amelazimika kutangaza uamuzi huo punde baada ya kuanza kesi hiyo kufuatia fujo zilizozuka mahakamani kutokana na mawakili wa familia za watu waliouawa katika vuguvugu la mapinduzi nchini Misri kupinga uhalali wa jaji huyo kusikiliza kesi hiyo. Jaji Mostafa Abdullah aliwahi kusikiliza kesi iliyojulikana kama Vita vya Ngamia na kuwatoa hatiani washtakiwa wote waliotuhumiwa kuhusika na mauaji ya waandamanaji. Kesi ya Hosni Mubarak itasikilizwa na mahakama ya rufaa katika tarehe itakayotangazwa hapo baadaye. Katika kesi hiyo anakabiliwa na mashtaka ya kufumbia macho mauaji ya waandamanaji zaidi ya 840 wakati wa kipindi cha siku 18 za wimbi la mapinduzi yaliyouangusha utawala wake wa kidikteta. Mubarak alifikishwa mahakamani leo pamoja na wanawe wawili wa kiume Alaa na Jamal wanaokabiliwa na mashtaka ya ufisadi …/

0 comments:

Post a Comment