Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Friday 19 April 2013

Israel yashindwa kuzuia miradi ya nyuklia Iran

                     10Jumaadal Aakhir,1434 Hijiriyah/ April 20,2013 Miyladiyah
 Ehud Olmert Waziri Mkuu wa zamani wa utawala wa Kizayuni wa Israel amekiri kwamba, mikakati kadhaa ya kigaidi iliyofanywa na utawala huo dhidi ya miradi ya nyuklia ya Iran iligonga mwamba. Kwenye mahojiano aliyofanyiwa na gazeti ka Kizayuni la Israel la 'Jerusalem Post' waziri mkuu huyo wa zamani wa Israel amekiri kufeli njama za siri za utawala wa Israel zilizokuwa na lengo la kukwamisha kabisa miradi ya nyuklia ya Iran. Olmert amesema kuwa, kwa miaka kadhaa sasa Israel imekuwa ikifanya mikakati ya kukwamisha miradi ya nyuklia ya Iran, lakini kwamba Marekani ilipaswa kuchukua uongozi wa mikakati hiyo ya kuvuruga miradi ya nyuklia ya Iran. Inafaa kuashiria hapa kuwa, katika miaka ya hivi karibuni idadi ya wasomi na wataalamu kadhaa wa nyuklia wa Iran wameuawa kigaidi na vibaraka wa utawala wa Kizayuni na mashirika ya kijasusi ya nchi za Magharibi, amma miradi ya nyuklia ya Iran bado iko kwenye mkondo uleule wa kuiwezesha Iran kujipatia nishati ya nyuklia kwa malengo ya amani. Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Nyuklia IAEA umethibitisha mara kadhaa kwamba,  hakuna dalili zozote zinazoonyesha kuwa Iran inataka kutengeneza bomu la nyuklia.

0 comments:

Post a Comment