Duru za habari kutoka Israel, zinaarifu kuwa utawala wa Kizayuni
unaozikalia kwa mabavu ardhi za Palestina, umepatwa na kigugumizi baada
ya ngao yake ya makombora ijulikanayo kama 'Kuba la Chuma' kushindwa
kuzuia makombora ya wanamapambano wa Palestina. Hali hiyo imedhihiri
baada ya kuanguka makombora katika kitongoji cha Eilat yakitokea eneo la
Sinai, Misri. Hii ni katika hali ambayo, hivi karibuni Israel
ilitangaza ripoti zilizosisitiza kuwa, ilikuwa imeeweka Kuba la Chuma la
kuzuia makombora katika mji huo, baada ya kuwepo kwa tishio la
kutekelezwa mashambulizi ya makombora. Hata hivyo hapo juzi utawala huo
ulitangaza kuwa, rada zake zilikuwa zimegundua makombora yaliyokuwa
yanaelekea katika eneo hilo, hali iliyoufanya upige ving'ora vya hatari,
huku ngao yake ya makombora ya 'Kuba la Chuma' ikishindwa kufyatua
makombora ya kuyazuia makombora hayo. Kufuatia hali hiyo, utawala huo
bandia umejitetea kwa kusema kuwa, kuba lake la chuma halikufyatua
kombora la kutungua kutokana na sababu za kijografia. Hali hiyo
imewafanya walowezi wa Kizayuni kuishi katika hali ya wasiwasi mkubwa
baada ya kufahamu kuwa, kuba hilo lililokuwa likipigiwa upatu na Tel
Aviv, haliwezi kuzuia kishindo cha makombora ya muqawama unaouzunguka
utawala huo bandia.
Sikiliza Live
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment