Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Thursday 18 April 2013

Israel yapata kigugumizi kuhusu Kuba la chuma

Duru za habari kutoka Israel, zinaarifu kuwa utawala wa Kizayuni unaozikalia kwa mabavu ardhi za Palestina, umepatwa na kigugumizi baada ya ngao yake ya makombora ijulikanayo kama 'Kuba  la Chuma' kushindwa kuzuia makombora ya wanamapambano wa Palestina. Hali hiyo imedhihiri baada ya kuanguka makombora katika kitongoji cha Eilat yakitokea eneo la Sinai, Misri. Hii ni katika hali ambayo, hivi karibuni Israel ilitangaza ripoti zilizosisitiza kuwa, ilikuwa imeeweka Kuba la Chuma la kuzuia makombora katika mji huo, baada ya kuwepo kwa tishio la kutekelezwa mashambulizi ya makombora. Hata hivyo hapo juzi utawala huo ulitangaza kuwa, rada zake zilikuwa zimegundua makombora yaliyokuwa yanaelekea katika eneo hilo, hali iliyoufanya upige ving'ora vya hatari, huku ngao yake ya makombora ya 'Kuba la Chuma' ikishindwa kufyatua makombora ya kuyazuia makombora hayo. Kufuatia hali hiyo, utawala huo bandia umejitetea kwa kusema kuwa, kuba lake la chuma halikufyatua kombora la kutungua kutokana na sababu za kijografia. Hali hiyo imewafanya walowezi wa Kizayuni kuishi katika hali ya wasiwasi mkubwa baada ya kufahamu kuwa, kuba hilo lililokuwa likipigiwa upatu na Tel Aviv, haliwezi kuzuia kishindo cha makombora ya muqawama unaouzunguka utawala huo bandia.

0 comments:

Post a Comment