Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad
amesema Serikali italazimika kuchukua hatua za dharura katika
kukabiliana na wafanyabiashara wa dawa za kulevya nchini.
Alisema wafanyabiashara hao wamekuwa wakiwatumia
vijana kwa ajili ya kununua na kusambaza dawa za kulevya, bila ya
kuzingatia athari zitokanazo na biashara hiyo haramu ambayo pia
huzorotesha maendeleo ya kiuchumi kwa taifa.
Maalim Seif alieleza jhayo jana ana katika hafla
ya ufunguzi wa kampeni ya kupunguza matumizi ya dawa za kulevya na
athari zake shuleni, iliyofanyika Shule ya Sekondari ya Lumumba.
Alisema hatua za dharura ni lazima zitumike katika
kuwashughulikia wafanyabiashara hao, vyenginevyo taifa litaendelea
kuangamia kutokana na matumizi makubwa ya dawa za kulevya.
Alifahamisha kuwa wafanyabiashara wa dawa za
kulevya wamekuwa wakijali zaidi maslahi yao, na kuamua kuwatumia vijana
kuendeleza biashara na matumizi ya dawa hizo, jambo ambalo halikubaliki
kwa mustakbali wa Zanzibar.
Aliwahadharisha vijana kuwa makini na
wafanyabiashara hao na kutokubali kutumiwa katika biashara hiyo.
Ufunguzi wa kampeni hiyo iliyoandaliwa na “Sober Houses” chini ya
ufadhili wa Hoteli ya “Double Tree Tanzania”, ulikwenda sambamba na
uzinduzi wa chapisho maalum la kitabu ambacho kitatumika kufundishia
shuleni.
0 comments:
Post a Comment