12Jumaadal Aakhir,1434 Hijiriyah/ April 22,2013 Miyladiyah
Kundi la Boko Haram ambalo lilihusika na kuwateka nyara raia saba wa
Ufaransa limesema kuwa, kuachiwa huru raia hao ni ishara ya juhudi za
kundi hilo za kutaka kufanya mazungumzo na serikali ya Nigeria. Muhammad
Marwan mwanachama wa kundi la uasi la Boko Haram la nchini Nigeria
ametangaza kuwa kitendo cha kuwaachia huru raia saba wa Ufaransa ambao
walitekwa nyara tangu miezi iliyopita huko kaskazini mwa Cameroon karibu
na mpaka na Nigeria, kunaonyesha kuwa kundi hilo lina nia ya kufanya
mazungumzo na serikali. Marwan amesisitiza pia kwamba, kuachiwa huru
raia hao wa Ufaransa kumekuja baada ya mashauriano kati ya wakuu wa Boko
Haram kama juhudi za kuanzisha mazungumzo na kurejesha utulivu huko
Nigeria. Siku kadhaa zilizopita Rais Goodluck Jonathan wa Nigeria
alisema kuwa kumeundwa kamati ya watu 26 waliopewa jukumu la kuchunguza
uwezekano wa kuwasamehe wanachama wa kundi la Boko Haram kwa shabaha ya
kurejesha amani nchini humo.
Sikiliza Live
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment