Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Sunday 21 April 2013

Boko Haram yataka kufanya mazungumzo na serikali

                         12Jumaadal Aakhir,1434 Hijiriyah/ April 22,2013 Miyladiyah
 Kundi la Boko Haram ambalo lilihusika na kuwateka nyara raia saba wa Ufaransa limesema kuwa, kuachiwa huru raia hao ni ishara ya juhudi za kundi hilo za kutaka kufanya mazungumzo na serikali ya Nigeria. Muhammad Marwan mwanachama wa kundi la uasi la Boko Haram la nchini Nigeria ametangaza kuwa kitendo cha kuwaachia huru raia saba wa Ufaransa ambao walitekwa nyara tangu miezi iliyopita huko kaskazini mwa Cameroon karibu na mpaka na Nigeria, kunaonyesha kuwa kundi hilo lina nia ya kufanya mazungumzo na serikali. Marwan amesisitiza pia kwamba, kuachiwa huru raia hao wa Ufaransa kumekuja baada ya mashauriano kati ya wakuu wa Boko Haram kama juhudi za kuanzisha mazungumzo na kurejesha utulivu huko Nigeria. Siku kadhaa zilizopita Rais Goodluck Jonathan wa Nigeria alisema kuwa kumeundwa kamati ya watu 26 waliopewa jukumu la kuchunguza uwezekano wa kuwasamehe wanachama wa kundi la Boko Haram kwa shabaha ya kurejesha amani nchini humo.

0 comments:

Post a Comment