Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Sunday 21 April 2013

AZAM YASHINDWA KUFURUKUTA KATIKA UWANJA WA NYUMBANI

                               11Jumaadal Aakhir,1434 Hijiriyah/ April 21,2013 Miyladiyah

Mechi kali ya kombe la shirikisho baina ya Azam fc ya Tanzania dhidi ya timu ya jeshi la Morroco AS FAR Rabat imemalizika uwanja wa taifa jijini Dar es salaam kwa matokeo ya suluhu pacha ya bila kufungana.
Katika mchezo huo timu zote mbili zimekosa nafasi nyingi za kutia mpira nyavuni huku dakika za mwisho waarabu wa Morroco wakijiangusha mara kwa mara kutaka suluhu ugenini.
 Azam FC imeshindwa kutamba katika mchezo huo uliochezeshwa na mwamuzi Emile Fred kutoka Shelsheli na endapo ingeshinda ingejiwekea mazingira mazuri ya kusonga mbele hatua ya makundi.
 Sasa Azam watakuwa na kibarua kizito huko kaskazini mwa Afrika wiki mbili zijazo kwani watahitaji ushindi tu na si vinginevyo.
Kama wawakilishi hao watanzania watahitaji kujaribu bahati yao watahitaji kulazimisha suluhu ugenini ili sheria itumike, lakini kama watahitaji kusonga mbele ndani ya dakika 180 watalazimika kupata matokeo ya ushindi.
Katika dakika ya mwisho ya mchezo huo nyota wa Azam Kipre Herman Tchetche alipiga bunduki moja iliyogonga mtambaa panya na baada ya hapo mwamuzi Fred alipuliza kipenga cha mwisho kuashiria ngoma imemalizika.
Akiongea baada ya mechi hiyo kocha mkuu wa Azam fc, mwingereza Sterwat John Hall alisema ni matokeo mabaya kwao kwani wanahitaji kujipanga vizuri mechi ya marudiano.
“Tumepoteza nafasi nyingi, bahati haikuwa yetu lakini tunaweza kubadili matokeo tukienda kwao kwani katika soka kila kitu kinawezekana”. Alisema Hall.
Kocha huyo aliongeza kuwa timu yake ilicheza vizuri na kwa umakini sana lakini bahati haikuwa yao kwa siku ya leo. Chanzo Mjengwa blog

0 comments:

Post a Comment