Walowezi wa Kizayuni wameubadilisha msikiti mmoja wa kihistoria
ulioko Baitul Muqaddas na kuufanya Sinagogi. Taasisi ya Wakfu na Turathi
za Kihistoria ya al Aqsa imetangaza leo kuwa, walowezi wa Kizayuni
wameushambulia Msikiti wa kihistoria wa Hadhrat Daud AS huko Baitul
Muqaddas na kuiharibu vibaya sehemu moja ya msikiti huo na sehemu
iliyobaki imefanywa maabadi ya Mayahudi. Taasisi hiyo imeeleza kuwa,
wiki iliyopita walowezi wa Kizayuni wenye misimamo mikali wakisimamiwa
na askari wa wa Israel waliushambulia na kuuharibu msikiti mwingine wa
kihistoria uliojengwa katika karne ya 17 katika eneo la Aal Adajani huko
kusini magharibi mwa Masjidul Aqswa na ghorofa ya kwanza ya msikiti huo
imefanywa Sinagogi. Taasisi hiyo imeeleza kuwa, vitendo hivyo vya
walowezi wa Kiyazuni ni sehemu ya siasa za kutaka kuliyahudisha eneo
lote la Baitul Muqaddas kwa kufuta kabisa sura ya Kiislamu katika mji
huo.
Takwimu zilizotolewa na Taasisi ya Wakfu na Turathi za Kihistoria ya al Aqswa zinaonesha kuwa, tokea utawala wa Kizayuni wa Israel ulipoanza kuzikalia kwa mabavu ardhi za Palestina kwa lengo la kuziyahudisha, umeharibu zaidi ya misikiti elfu moja.
Takwimu zilizotolewa na Taasisi ya Wakfu na Turathi za Kihistoria ya al Aqswa zinaonesha kuwa, tokea utawala wa Kizayuni wa Israel ulipoanza kuzikalia kwa mabavu ardhi za Palestina kwa lengo la kuziyahudisha, umeharibu zaidi ya misikiti elfu moja.
0 comments:
Post a Comment